JINSI NILIVYOFAULU
1.
Jiwekee
lengo moja kubwa ambalo utalifanyia kazi kila siku.
2.
Kila siku kazana kuwa bora zaidi ya jana,
shindana na wewe mwenyewe na siyo mtu mwingine.
3.
Kwenye
kila kipato unachoingiza, tenga asilimia 10 na weka pembeni kabla hujaanza
kutumia.
4.
Asilimia 10 unayoiweka pembeni, iwekeze sehemu
ambayo inazalisha zaidi.
5.
Punguza sana au acha kabisa kutumia mitandao
ya kijamii kama haikuingizii kipato.
6.
Usianze
siku yako kwa kufuatilia habari.
7.
Amka mapema zaidi ya ulivyozoea, angalau saa
moja na tumia muda huo kusali/kutahajudi, kujisomea na kufanya mazoezi.
8.
Pangilia siku yako kabla hujaianza, tafakari
siku yako kabla hujaimaliza.
9.
Weka muda kwenye kujenga mahusiano yako, hasa
ya wale wa karibu.
10. Weka juhudi zaidi kwenye kazi/biashara, nenda
hatua ua ziada kwa kila unachofanya.
11. Usitoe ushauri kwa mtu ambaye hajakuomba,
usichukue ushauri kwa ambaye hujamwomba.
12. Usijisumbue kuwabadilisha watu, watu huwa
hawabadilishwi.
13. Shukuru kwa kila jambo, pokea kila hali
unayokutana nayo na igeuze kuwa bora.
14. Usilalamike wala kumlaumu yeyote kwa chochote,
beba jukumu la maisha yako.
15. Fanya kilicho sahihi mara zote na siyo kilicho
rahisi.
↓↓↓
Comments